Header Ads

BannerFans.com

Kumbe Azam fc imeipa ubingwa Simba fc msimu huu






Na mwenda plus

Msimu wa ligi kuu Tanzania bara2017/18  almaarufu VPL ukikaribia kufika ukingoni  uku kila timu kwenye ligi hiyoo  ikibakisha michezo michache na tayari  bingwa wa ligi hiyoo ameshapatikana ambayo ni timu ya soka ya simba sport club ya jijini Dar es salaam almaarufu   wekundu wa msimbazi wamechukua ubingwa huo kwa kujikusanyia  zaidi ya alama  68 nyuma ya mahasimu wao Azam fc wakiwa na alama 55 kibindoni wakifatiwa na yanga fc wakiwa na  alama 48 uku  maji maji fc, ndanda fc na njombe mji zikiwa hatarini kuteremka daraja.

 

Baadhi ya wadau wa soka  wametoa maoni  yao kuhusiana na mwenendo wa ligi nzima na kupongeza mabingwa wa msimu huu ambao ni simba fc kwakuonyesha kiwango kizuri cha soka na kupoteza  mchezo mmoja tu hadi sasa. Licha ya kandanda zuri walio onyesha pia simba msimu huu wamekua na kikosi  bora kabisa kikiongozwa na  mchezaji wa kimataifa kutokea Uganda  Emanuel Okwi akiongoza kwa magoli 20 akifatiwa na John Bocco akiwa na magoli 14.

Pia wadau wamezungumzia mbinu zilizopelekea Simba kupata ubingwa msimu huu kwanza kuwa na kikosi bora kabisa, uongozi bora na usajili bora ulio fanywa na mabingwa hao.

Ikumbukwe simba wamefanya usajili msimu huu kwa kuwachukua  wachezaji wanne kutoka Azam fc akiwemo John Bocco, shomar Kapombe, Aishi Manula na Erasto Nyoni waliopelekea wekundu hao kupata ubingwa. Wachezaji hao wa Azam wamechangia kwa kiasi kikubwa kwa klabu hiyo kupata ubingwa kutokana na unyumbulifu wao wakiwa uwanjani na hata mwalimu wa timu hiyo Pierre Lechantre kuwafanya ni chaguo  la kwanza kwa kila mchezo watakao cheza katika kikosi chake.

Ni wazi kabisa Azam fc ndio waliochangia kwa kiasiki kubwa kwa simba fc, kupata ubingwa msimu huu kutokana  na  kuwa ruhusu  wachezaji hao wa nne kwenda simba bila ya kuangalia  uwezo na  ubunifu waliokuwa nao wachezaji hao pindi wanapokuwa uwanjani na kuwafanya  simba  kuwa na kikosi kipana kilicho wawezesha simbakunyakua ubingwa msimu huu.
Hata hivyo ubora wao Simba auja jidhihirisha kuchukua ubingwa msimu huu tu bali na kuwa funga wahasimu wao wajadi  yanga fc, pindi walipokutana na Azam fc na kutoa mchezaji aneongoza kwa magoli hadi sasa.

Pia simba fc imekamilisha mchakato wake na kupitisha rasmi kwenye katiba  yao mgawanyo wa hisa wa klabu na muwekezaji. Katika mgawanyo huo  wa hisa  muwekezaji  ana chukua  asilimia 49 na klabu inabaki  na asilimi 51. Uku  waziri mwenye dhamana  na michezo Dr Mwakyembe akibariki  mchakato huo.

Pia ikumbukwe Simba haijashinda ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara tangu walipofanya hivyo mara ya mwisho msimu wa 2011/12. Mpango pekee wa Simba kwa miaka ya hivi karibuni ni kushinda taji hilo ili kurejesha heshima Msimbazi.

No comments

Powered by Blogger.