Header Ads

BannerFans.com

Kipa wa Liverpool awaomba msamaha mashabiki kwa uzembe alioufanya jana dhidi ya Madrid

Champions League Final - Real Madrid v Liverpool - Niederlage für Liverpool (Imago/MIS/B. Feil)
Mlinda mlango wa Liverpool Loris Karius akitokwa na machozi baada ya makosa aliyofanya kuigharimu timu yake.

Mlinda mlango wa liverpool Mjerumani  Loris Karius  aliizawadia Real madrid  bao  la kuongoza  katika dakika  ya  51 wakati, alipojaribu  kuharakisha  kuanzisha mashambulizi, aliurusha  mpira mbele  ya  mshambuliaji  wa  Real Karim Benzema, ambaye  alinyoosha  mguu  wake na  kuuweka mpira  wavuni. karius , mwenye umri  wa  miaka  24 , pia alifanya makosa  katika  goli  la  tatu  la  Real  wakati Gareth  Bale  alijaribu kupiga  mpira  ya  mbali  ambao  ulijaa  wavuni baada  ya kumchoropoka  kipa  huyo  wa  Liverpool.
"Sijisikii  kitu  chochote sasa  hivi. Leo nimesababisha timu  yangu kupoteza  mchezo  na  najisikia  vibaya  sana  na  nasikitika  na kuomba  msamaha kwa  kila  mtu," Karius  alisema.
"Naomba  samahani  kwa  kila  mtu, kwa  timu, kwa  klabu , kwamba makosa hayo  yameigharimu  timu. Iwapo  ningerudisha  nyuma muda , ningeweza. Nina  masikitiko  makubwa  kwa  timu  yangu. Nafahamu  nimewaangusha  leo.
"Magoli  haya  yametugharimu  kukosa  ushindi, kimsingi," aliongeza.
Champions League Final - Real Madrid v Liverpool - Niederlage für Liverpool (Imago/VI Images/M. Steen) Mlinda mlango wa Liverpool Karius akilala chini kwa uchungu baada ya kufanya makosa mawili yaliyosababisha madhara makubwa kwa timu yake.
"Ni vigumu  kwa  sasa  lakini  hayo  ndio  maisha  ya  mlinda  mlango. Unapaswa  kuinua  kichwa  chako juu  tena."

No comments

Powered by Blogger.