Header Ads

BannerFans.com

Mahakama yaamuru marekebisho kesi ya mbowe na vigogo wengine wa chadema




Dar es salaam. Mahakama ya hakimu mkazi kisutu imeamuru upande wa Mashtaka kufanya marekebisho katika hati ya mashtaka yanaomkabili mwenyekiti wa cha Chadema, Freeman Mbowe na vigogo wengine nane wa chama hicho

Uamuzi huo umetolewa leo jumatatujuni 11,2018 na Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri.
Baada ya kutoa uamuzi huo, wakili wa utetezi peter kibatala alielezea mahakamani hapo kuwa  hawajaridhishwa na uamuzi huo na akawasilisha taarifa  ya kusudio la kukata rufaa.

Hakimu mashauri alitoa uamuzi huo baada ya kupitia mapingamizi nane yaliyowasilishwa mahakamani hapo na kibatala na jeremiah Mtobesya.

Kwa pamoja kesi hiyo, hakimu Mashauri alikubaliana na baadhi ya hoja za upande wa utetezi kuwa katika shtaka la pili,tatu, nne, tano,sita na saba yana upungufu wa kisheria na kuamuru upande wa mashtaka kufanya mabadiliko katika hati ya  mashataka.

Baada ya kutoa uamuzi huo, wakili kibatala aliieleza mahakama kuwa hawajaridhishwa na uamuzi huoo hivyo aliwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa

Kibatala amedai kuwa wanakata rufaa kwa sababu wao waliomba  mashtaka hayo yafutwe lakini Mahakama imeamua yafanyiwe marekebisho kwenye hati ya mashtaka.

Baada ya kibatala kueleza hayo, wakili waserikali, Paul  Kadushi amedai kuwa  huo ni uamuzi mdogo ambao hauwezi kumaliza kesi na kwamba uamuzi huo hawawezi kuukatia rufaa. Kibatala amesisitiza kuwa kwa kuwa Mahakam  imeona mashtaka hayo  ni batili

No comments

Powered by Blogger.