Header Ads

BannerFans.com

Algeria ya watelekeza wahamiaji

Algerien Geflüchtete in Wüste ausgesetzt (picture-alliance/dpa/J. Delay)
Katika miezi 14 iliyopita, Algeria imewatelekeza wahamiaji wapatao 13,000 miongoni mwao wanawake waja wazito na watoto. Mamia ya wahamiaji waliofukuzwa wanateseka kwenye jangwa la Sahara bila chakula au hata maji.

Wengi wa wahamiaji hao hutokea nchini Niger, ambapo wale waliobahatika huvuka eneo lisilokuwa na mwenyewe lenye umbali wa kilomita 15 na kuingia katika kijiji kidogo cha Assamaka. Mwakilishi wa shirika la kimataifa la uhamiaji IOM Alhoussan Adouwal ameeleza kuwa wahamiaji hao mara nyingi huachwa umbali wa kilomita 15 na kutokea hapo wanatembea kwa miguu hadi Assamaka. Wengi wa watu hao huhangaika na kuteseka kwa siku kadhaa kabla ya kufikiwa na kikosi cha waokoaji cha Umoja wa Mataifa. Idadi ya watu isiyojulikana pia huangamia kwenye safari za aina hiyo. Karibu manusura wote waliohojiwa na shirika la habari AP wameelezea juu ya watu katika makundi yao ambao hawakuweza kuendelea na safari na hatimae walipotea kwenye jangwa hilo la Sahara.

Tangu mwezi Oktoba mwaka jana Algeria imeongeza harakati zake ya kuwafukuza wahamiaji kwa sababu ya shinikizo kutoka nchi za Umoja wa Ulaya kwa nchi za Afrika Kaskazini juu ya kuwadhibiti wahamiaji wanaotaka kwenda barani Ulaya kupitia kwenye bahari ya Mediterania au kwa kupitia kwenye ukuta wa kizuwizi na Uhispania.

No comments

Powered by Blogger.